Sharon Bukokhe enzi za uhai wake.
Sharon Bukokhe akiwa kajipumzisha nyumbani kwake.
MREMBO Sharon Bukokhe, 28, Mkenya aliyehamia Uingereza, amejiua kwa
kujikuta akiishi katika upweke wakati familia yake imetawanyika sehemu
mbalimbali duniani.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na vyombo
husika, Bukokhe alijiua mwezi Aprili nyumbani kwake kutokana na familia
yake kuwa mbali naye, akiwemo mumewe ambaye yuko Afrika Kusini.
Sharon kabla hajaamua kuitoa roho yake.
Ujumbe aliouacha nyumbani kwake kabla ya kujiua ulisema: “Nafikiri
maisha yangu ni ya thamani kama yajayo, kwa vile kufa ukiwa na umri wa
miaka 25 ni sawa na kufa ukiwa na miaka 88. Sijutii au kuogopa
chochote, najiona nafanya haki tu.”
Mwanamke huyo aliyeonekana kuwa
“mwenye furaha zaidi duniani” kwa mujibu wa marafiki zake alihamia
Uingereza mwaka 2002 na akahitimu masomo kwenye chuo kikuu cha uhandisi
cha Nottingham Trent nchini humo.
Mama yake anaishi Marekani na dada
yake yuko Canada, ambapo kaka yake yuko Gillingham, Kent, Uingereza
lakini kwa umbali wa kilomita 402 kutoka alipo.
Alipohitimu chuo kikuu Uingereza.
Picha nyingine enzi za uhai wake akiwa katika vazi murua.