flash3

Thursday 2 August 2012

HII NDIO PICHA YA KWANZA KUMUONA SNOOP DOGG BAADA YA KUTANGAZA KUIMBA REGGAE!



Inawezekana kuwa ni njia mpya ya kutaka kuteka watu nyara na kutengeneza hela kwa aina mpya ya biashara baada ya kukaa kwenye muziki kwa miaka ishirini, huu ni uamuzi wa rapper Snoop Dogg ambaye sasa amebadilisha jina na kujiita Snoop Lion.
Ametangaza kuanza kuimba muziki wa Reggae anaouita muziki wa upendo, muziki atakao kuwa huru kuuperform hata kwa bibi, babu na watoto kwa sababu una mapokezi kwa marika yote tofauti na muziki wake wa kigumu alioufanya kabla.
Snoop Lion amesema alichofahamu kutoka kwa Marasta ni kwamba sio dini kama watu wanavyofikiria pia kuhusu jinsi wanavyoishi, amegundua kitu kingine tofauti pamoja na kusisitiza kwamba amekuwa na rasta kwa kipindi kirefu lakini alikuwa hajafungua jicho la tatu ili kuligundua hilo, ila baada ya kufungua ndio amefahamu.
(picha zake za awali kabla ya maamuzi yake ya kufanya muziki wa rege.)
Kubadili jina na kuanza kufanya muziki wa Reggae hakuwa amekupanga, anasema ni hisia zilikuja tu na akaamua kuzifata, baada ya hapo ndio akasafiri mkapa Jamaica na kuingia kwenye studio ambayo aliiagiza imtengenezee kazi za ukweli za Reggae ambazo alizifurahia na kuzifanyia kazi.
Snoop mwenye umri wa miaka 40 ambae kipimo cha DNA kilionyesha kwamba asili yake sio Asia bali ni Africa 75%, 23% Native American na 6% European amesema haimaanishi kwamba muziki wa rap aliokuwa akiufanya mwanzo ni mbaya na kwamba anauacha bali anafanya muziki ulio kwenye hisia zake kwa sasa ambao ni reggae.

No comments:

Post a Comment