flash3

Wednesday 9 May 2012

BEYONCE ASEMA ANAHITAJI WATOTO ZAIDI.

Mama wa mtoto mmoja Beyonce jumatatu alikuwa kwenye GLAMOROUS MET GALA huko New York, Kutoka Entertainment tonight Nancy O’Dell alimpiga Beyonce picha akiwa red carpet akiwa anafanya mahojiano, huku akiwa amevalia gauni refu jeusi. Beyonce mwenye miaka 30 alimuongelea mtoto wake wa miezi minne Blue Ivy Carter ambaye alikuwa nyumbani na baba yake Jay Z na mama yake Tina Knowles.Alisema anataka kuongeza mtoto mwingine kwenye familia lakini huenda isitokee siku za karibuni “Hata hivyo nataka watoto zaidi, sijui wangapi lakini Mungu ndo anajua” Alisema Beyonce. Beyonce atarudi kwenye satge kwa mara ya kwanza karibu mwaka sasa na series shows kwa dola bilioni 2.4 Revel Resort katika Memorial Day Weekend na show ya nne imewekwa kuwa Jumatatu Mei 28.

Liverpool manager Kenny Dalglish satisfied with first full season...........

Manager Kenny Dalglish said it had been "not a bad" first full season back at Liverpool after their home campaign ended with victory over Chelsea.
Dalglish's team won the Carling Cup, securing a place in the Europa League, and reached the FA Cup final.
"We've got a bit of silverware back in the cupboard after six years; we're back in Europe at the first time of asking," said Dalglish.
"We were near to winning the FA Cup final. Not a bad first season."
Dalglish returned for a second spell as Liverpool manager following the departure of Roy Hodgson in January 2011 and signed a three-year deal last summer.
However, his team won just six of their 19 home games in the Premier League this campaign and did not win a league fixture at Anfield between 30 December and 13 March.
They went into Tuesday's match at Anfield on the back of two successive defeats, but triumphed 4-1 against a Chelsea team much-changed from that which won Saturday's FA Cup final at Wembley.
"I think the players will be happy to finish on a high at Anfield," said Dalglish.
"That performance was on a par with a lot of other performances where we've not had the result. Against Chelsea we got that."
Michael Essien's own goal gave the hosts the lead, with goals from Jordan Henderson and Daniel Agger making it 3-0 in a first half that also saw Stewart Downing hit the post with a Liverpool penalty.
Ramires bundled in early in the second half to reduce the arrears, but Jonjo Shelvey restored the three-goal margin by firing in from long range after being gifted possession by Chelsea keeper Ross Turnbull. 
Liverpool's 24 goals at home equals their lowest tally for a season, which they recorded in 1903-04
With the score 0-0, Chelsea's Branislav Ivanovic hit the post with a header and Fernando Torres struck the bar later in the half, while Downing was also denied by the woodwork.
"I have said many times this season how well we've played but not had the break to win it," added Dalglish.
"On this occasion, maybe with Branislav Ivanovic hitting the post for Chelsea early on, we thought we might have got that bit of luck.
"I don't think it was luck that got us the victory, though. It was a fantastic performance from everyone.
"The two young lads, Shelvey [20] and Henderson [21], in the middle of the pitch were fantastic with the work-rate they got through and both of them scored too.
"It was the same with Luis Suarez and Andy Carroll up front, and I don't know how neither of them scored. Luis was fantastic for our first goal but so was everyone.
"We had a good day and it was an excellent performance."
The win lifted Liverpool up to eighth in the Premier League table, and ensured they have the chance to climb further up the table - and overhaul local rivals Everton - when their season ends at Swansea on Sunday.

BABA ATOBOA SIRI YA KILICHOMPONZA KANUMBA

Mohammed Kuyunga na Joseph Shaluwa HUKU wingu zito likiwa bado limetanda juu ya kifo cha stadi wa filamu za Kibongo, Steven Charles Kanumba, baba mzazi wa marehemu, Mzee Charles Kusekwa ameibuka na kueleza mazito aliyoyataja kama ndiyo yaliyomponza mwanaye, Risasi Mchanganyiko linakujuza.
Akizungumza kwa njia ya simu wikiendi iliyopita kutokea Shinyanga, Mzee Kusekwa alisema wanaomtuhumu kuhusika na kifo cha mwanaye wanakosea kwa vile kuna jambo jingine nyuma ya pazia.

MWANZO WA JAMBO LENYEWE
“Ni vigumu kwa mtu ambaye una mtoto mkubwa unayemtegemea katika maisha halafu ushiriki kumfanyia mambo ya kishirikina, hilo haliwezekani hata siku moja.
“Watu wanatumia kigezo cha kuhitilafiana na mwanangu kuwa sababu ya kunihusisha na kifo chake. Yule ni mwanangu hata iweje, mtoto akikuchafua mkono kwa kinyesi huwezi kuukata mkono, hayo yalishapita sioni sababu ya kutaka kuhusishwa na kifo hicho.”

AANZA KUFUNGUKA
Akienda mbali zaidi, mzee huyo alisema tatizo lilisababishwa na tambiko ambalo yeye aliliita haramu kwa sababu halikuwahusisha wazee wa kimila wala kufuata taratibu zinazotakiwa.
Alisema, tatizo ni kijana aitwaye Ayubu Mujungu ambaye ni mpwa wake (mtoto wa dada yake mzee huyo) aliyemchukua marehemu Kanumba na kumpeleka kwenye kaburi la babu yake kutambika kinyume na utaratibu wa mila zao.
“Kama ni matatizo ameyasababisha Ayubu ambaye kwa ujeuri tu alimchukua marehemu na kumpeleka Simiyu kwa ajili ya kutambika katika makaburi ya wazazi wangu.
“Binafsi miye na wazee wenzangu tulishangaa kuona kijana huyo akimchukua mtoto mwenziye (Kanumba) na kwenda naye kutambika katika makaburi bila ya kuwajulisha wazee.
“Kikwetu suala la matambiko hufanywa kwa taratibu maalum tena chini ya usimamizi wa wazee. Siyo mtu yeyote anaweza kwenda kufanya tambiko,” alisema.

ALIKIUKA MASHARTI
Alisema jambo jingine linalomfanya ahusishe tambiko la Kanumba na Ayubu katika kifo hicho ni kitendo cha marehemu kukiuka masharti ya kufanya tambiko kwa kuvaa mavazi siyo.
“Kuna kosa lingine Kanumba alilifanya, alivaa nguo nyeusi ambazo wazee wanasema kuwa haziruhusiwi kwenda nazo huko,” alisema.
Mzee Kusekwa alisema kuwa matokeo ya kukiuka mavazi, baada ya Ayubu na Kanumba kufika makaburini walikutana na vitu vya ajabu ambavyo mpaka leo ni Ayubu tu ndiye anayevijua lakini hataki kuviweka wazi.
Alizidi kuweka wazi kuwa ili kuwafunga midomo watu waliokuwa kwenye eneo la makaburi na kushuhudia maajabu yaliyowatokea wawili hao, waliwapa shilingi laki moja ili wasiseme.
“Hicho ndicho kilichosababisha kifo cha Kanumba kwa kuwa walikwenda kufukia vitu kwenye kaburi. Baada ya tukio lile mwanangu aliporejea Dar ndiyo akapata matatizo,” alisema.
KUHUSU MALI ZA KANUMBA
Mzee Kusekwa alisema muda wowote wiki hii atatua jijini Dar es Salaam kufuatilia suala la mali za mwanaye ambazo anadai amesikia zimeanza kuuzwa kiaina.
“Kuna kesi nimefungua Mahakama Kuu kuhusu kuzuia mali za mwanangu kuuzwa, hilo ndilo haswa linalonileta Dar. Kuna watu wanasema eti kwa mila za Kisukuma sistahili kuwa mrithi kwa sababu sikumtolea mahari mama Kanumba, hao wanakosea sana.
“Duniani kote watu wameshindwa kufananisha thamani ya fedha na uhai wa mtu, hakuna anayejua thamani ya mbegu ya Kanumba, hivyo kama sikumtolea mahari mama yake siyo sababu ya kunizuia kurithi mali za mwanangu. Mimi ndiye msimamizi wa mirathi,” alisema.

AMCHAMBUA AYUBU
Mzee Kusekwa alisema, chokochoko zote hizo amezileta Ayubu ambaye ni mtoto mdogo, akasema yeye (Ayubu) hajui mzee huyo na mama Kanumba walikutana wapi na walioana au hawakuoana.
Ameongeza kuwa Ayubu ni mtu wa kuchunga sana kwa kuwa tayari ameshajipendekeza kwa mama wa marehemu ili atajwe kama msimamizi wa mirathi wakati si mtu wa ukoo wao.

AMSHAURI MAMA KANUMBA
Katika kile kilichoonekana kutuliza hali ya hewa, mzee Kusekwa alitoa maneno aliyosema kuwa ni ushauri kwa mzazi mwenzake, Flora Mtegoa.
“Namsihi mzazi mwenzangu asisikilize maneno ya Ayubu maana ni mchonganishi, sisi tulishafanya kikao cha wanandugu lakini hakutokea, tukamtafuta na polisi kutokana na maneno yake akajificha uvunguni, bahati mbaya hatukuwa na hati ya kuingia ndani,” alisema na kuongeza:
“Aache kuamini ushirikina kwa kusema mtoto amechukuliwa msukule, hakuna msukule hapo ni matatizo ya tambiko. Kikubwa kwake kwa sasa ni kujenga imani kwa Mungu kwa kuwa ndiye aliyemchukua kiumbe wake.”

AYUBU KIKAANGONI
Risasi Mchanganyiko lilimtafuta Ayubu kwa njia ya simu na kuzungumza naye kuhusiana na madai hayo ya mjomba wake ambapo alitoa ushirikiano wa kutosha.
Kwanza, alianza kwa kukiri kuongozana na merehemu Kanumba kwenye makaburi yanayozungumziwa, akasema aliyewaagiza kufanya hivyo ni mama wa staa huyo Bi. Mtegoa.
“Tangu mwaka jana, mama Kanumba aliniagiza nimpeleke ndugu yangu katika makaburi na siyo kutambika bali ni kwenda kuyafagilia, hivyo Machi mwaka huu ndiyo tukatimiza,” alisema.
Kuhusu kutokewa na kitu kibaya makaburini hapo, alikanusha ingawa alikiri kumpatia fedha dada yake anayemfuata aitwaye Lucy ambaye ni mlemavu wa miguu.
“Hatukuwa tunamhonga, hapana. Yule ni dada yangu, tena anayenifuata mimi, tuliamua kumpa fedha kwa ajili ya kujikimu. Hata hivyo si laki moja kama alivyosema mjomba, ilikuwa ni shilingi 80,000.
“Tena nakumbuka mimi nilitoa 50,000 na Kanumba akatoa 30,000 fedha ambazo hazikuwa na sharti lolote lile.”

KUHUSU KANUMBA KUVAA NGUO NYEUSI
“Kanumba alivaa suruali ya jeans, rangi siikumbuki vizuri lakini haikuwa nyeusi na shati la rangi ya kaki. Hakuvaa nguo nyeusi kabisa.”
Madai ya mzee Kusekwa kuwa anajipendekeza ili awe mrithi wa mali za marehemu Kanumba, Ayubu alisema si ya kweli na kwamba amejijenga vizuri kimaisha na si kutegemea mali za urithi.
“Nina pikipiki, gari, nyumba na ninaendesha biashara zangu mwenyewe, sina shida na mali za marehemu. Kwanza nafahamu kuwa mwenye haki ya kurithi ni mama mzazi wa Kanumba.
“Hata huko kuondolewa katika ukoo ni watu wachache tu waliokutana kutokana na ushawishi wa baba Kanumba na sijapewa taarifa yoyote kwa kuwa aliyepangwa kuniambia, Elius Meshack hajaniambia chochote mpaka sasa.”
Ayubu alisema anashukuru kuwa yeye amemzika ndugu yake, amemuona kwa mara ya mwisho wakati alipomvalisha nguo na kumuwekea Biblia katika jeneza lake.

MAMA KANUMBA ANENA YAKE
Katika hatua nyingine, mama mzazi wa marehemu amezungumza kuhusu suala la mzazi mwenzake kuharakisha suala la mali za Kanumba huku akisisitiza ni mapema sana.
Akizungumza kwa uchungu, nyumbani kwa marehemu Sinza jijini Dar es Salaam wikiendi iliyopita, mama huyo alisema mzazi mwenzake aache kuzungumzia kuhusu mali kwa wakati huu kwa vile ni mapema sana.
“Mimi nina uchungu na mwanangu, lakini mwenzangu naona anajali zaidi mali. Mimi ninalia, bado nipo kwenye msiba, yeye anasherehekea. Ndiyo maana hakuja msibani, mimi nimefika kumzika mwanangu, lakini siku chache baadaye, tayari anasema anazijua mali za marehemu.
“Sina haja na mali za Kanumba, nina nyumba, kazi na mali zangu nyingine, kwa nini nigombee mali? Nilitamani sana mwanangu anirithi mimi na siyo mimi nimrithi yeye.
“Ninatambua kuwa yeye ni baba wa marehemu, hilo halina ubishi, lakini atulie kwanza. Hata arobaini bado tunazungumzia mali, za nini? Halafu haya mambo yanakwenda kisheria, muda ukifika tutafungua mirathi mahakamani. Nipo tayari kusimama naye na siyo kulumbana kwenye magazeti,” alisema Flora.
Akaongeza: “Hata ukiangalia sababu ya kutokuja kumzika mtoto haikuwa na maana. Mimi nilipopata taarifa mara moja nilifika, lakini mwenzangu akasubiri kamati ya mazishi impatie utaratibu na nauli. Utawezaje kusubiri kamati wakati umefiwa na mwanao?
“Kitu cha kushangaza alitumiwa nauli lakini hakufika kwa visingizio ambavyo mimi naviona havina maana. Hebu angalia, mfano alisema eti anaumwa, mbona alitumiwa nauli ya ndege? Usafiri wa ndege una shida gani? Ndiyo maana mimi nasema wakati mimi maumivu yangu yakiwa kwenye msiba, mwenzangu anawaza kupata mali, sasa asubiri muda ufike.”
Bi. Flora alikuwa katika sura ya majonzi muda wote, alipokuwa akizungumza na mwandishi wetu, lakini hali ilibadilika ghafla katikati ya mahojiano baada ya ndugu zake waliofika kumpa pole nyumbani hapo.
Ni kama msiba ulianza upya, maana alishindwa kujizuia na kuangua kilio, hivyo kusababisha wageni hao kujumuika pamoja kulia.

KALAMU YA MHARIRI
Kanumba amefariki dunia, ameshazikwa. Hakuna wa kubadili ukweli huu. Ni vyema sasa wazazi wakakutana na kujadiliana pamoja kuhusu suala la mirathi na kuacha kutupiana lawama. Majadiliano yenye usawa ni bora zaidi ya malumbano.

Lukuvi: Hatuna takwimu za vifo kwa `Babu`

May 9, 2012
By
 Serikali ya Taifa la Tanzania imesema haina takwimu sahihi za vifo vya wagonjwa waliopoteza maisha kutokana na kukatisha dawa za kurefusha maisha baada ya kunywa kikombe cha Babu wa Loliondo, Mchungaji Ambilikile Mwasapile, na haijui alipo kwa sasa.
Mchungaji huyo kuanzia mwishoni mwa mwaka juzi na mwanzoni mwa mwaka jana alikuwa akitoa dawa ya miti shamba ambayo alidai inaponya magonjwa sugu ukiwemo Ukimwi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, jana alisema serikali yao haina taarifa za mchungaji huyo wala haijui takwimu sahihi za vifo vya wagonjwa walioacha dawa ya kurefusha  maisha ARVs baada ya kupata kikombe.
Lukuvi aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam, baada ya kufungua warsha ya viongozi wa dini na viongozi wa vyama vya siasa kuhusu mbinu za kupambana na ugonjwa wa Ukimwi.
“Ni kweli serikali ilikuwa inajua taarifa za mchungaji huyo, lakini kwa sasa haijui yupo wapi na anafanya nini labda waulizwe viongozi wake wa dini,” alisema.
Lukuvi alisema watu walioacha dawa ya kurefusha maisha baada ya kunywa kikombe walifanya makosa makubwa na kukiri kuwa wengi wao wameshapoteza maisha.

Tuesday 8 May 2012

Picha Za Siku Lo!!!.......
wanaume kazini....wayaweza haya mwanamume????

Monday 7 May 2012

Blackban Relegated

Blackburn have been relegated to the Championship after losing at home to Wigan, whose Premier League status is secure for next season.
Antolin Alcaraz headed the Latics to victory from a corner late on a rainy and rancorous night at Ewood Park.
Only a win would have given Rovers a chance of avoiding the drop but they were sloppy and shot-shy.
The visitors were lively in the first half, less so in the second, but took their chance to claim a decisive win. 
It is a remarkable sixth victory in eight games for the Latics and leaves them five points clear of the relegation zone with one game left to play.
The result brings about a disastrous conclusion to what has been a turbulent season for Blackburn and their manager Steve Kean and an end to their 11-year stay in the Premier League.
The Scot has regularly been the focal point for abuse from frustrated Rovers fans, unhappy with his management and the way the club is being run by the owners, Indian poultry firm Venky's.
This continued on Monday in the form of mass chanting throughout, a lone fan invading the pitch at the start of the second half and, presumably, the reason why a chicken draped in a Blackburn flag appeared in the Wigan box five minutes into the game and had to be caught by Latics goalkeeper Ali Al-Habsi.
The goal four minutes from time heightened calls for Kean's sacking and the exit of Venky's, which only increased when the final whistle blew to confirm Rovers' fate.
Venky's looked set to be rewarded for sticking with Kean when he led them six points clear of the drop zone following a win over Sunderland on 20 March, but a disastrous run of seven defeats in eight games since then has cost the club.
Their performance here was meek as they limped out of the division. It was only in the second half that they had any attacking impetus and even then this was only intermittently. 
Yakubu, who has been one of very few redeeming features of Blackburn's season, had a close-range volley blocked on the line and Junior Hoilett, their other shining light, was clearly caught by a swinging boot Emmerson Boyce, but when referee Mark Clattenburg waved away the penalty appeals, Rovers hopes were dented.
Blackburn's plight has been compounded by the form of Wigan, who were rock bottom when Rovers beat Sunderland but, in stark contrast to Kean's side, have been in scintillating form since late March, including hugely impressive victories over Manchester United, Arsenal and Newcastle.
The Latics' success is testimony to their manager Roberto Martinez, who has stuck to his passing principles, and owner Dave Whelan, who remained loyal to the Spaniard despite the threat of relegation.
The visitors were sharp throughout, zipping passes neatly around the increasingly wet surface and always looked the more likely to score.
Franco di Santo fired a good chance over, Victor Moses fluffed an even better chance from close range when he misjudged a header from Boyce's cross and Shaun Maloney spurned a header of his own from the same supplier.
In the end, though, none of these mattered as Alcaraz rose highest at the back post to power a header in from a corner to confirm his side's safety and send Rovers spinning into the second tier.

MAHAKAMA YATUPILIA MBALI OMBI LA LULU......

 Lulu (katikati) akiingia mahakamani na askari magereza wa k***.

Huku kesi ya inayomhusu Msanii wa filamu za maigizo nchini Tanzania, Elizabeth Michael ‘Lulu’, jana alipandishwa tena kizimbani mara ya tatu katika kesi ya mauaji ya Kanumba inayomkabili ambapo mawakili wanaomtetea wakiongozwa na Kennedy Fungamtama waliwasilisha ombi la kurekebisha umri wa mshitakiwa huyo kuwa miaka 17 na si 18 kama ilivyowasilishwa mahakamani hapo.Fungamtama na jopo lake walisema mteja wao ni mtoto mdogo hivyo kesi hiyo ipelekwe mahakama ya watoto na kuwasilisha cheti kinachoonesha ana umri wa miaka 17. Upande wa mashitaka umetupilia mbali ombi hilo na kudai cheti kilichowasilishwa kina mapungufu kadhaa likiwemo jina la Dyana ambalo halijawahi kusikika likitumiwa na mshitakiwa huyo.

 hatima yake ni gani mwana dada ,huyu jamani?

Big Brother Africa Star-game Launch Party:

 Usiku wa jana, jumba la Big Brother Africa lilifunguliwa rasmi tayari kuanza mchezo wa Stargame ambamo Mkenya mwenzetu Rapa CMB PREZOO aliliwakilisha taifa letu huku Jirani zetu Tanzania wakiwakilioshwa na, Hilda na Julio. Macelebs na waalikwa kibao walishiriki kwenye shughuli iliyoandaliwa na Multichoice Tanzania kuwasindikiza washiriki wao na kuwapa support.

DIAMOND ATOA MSAADA KATIKA KITUO CHA YATIMA

 ICON katika mziki wa Bongofleva Naseeb Abdul ‘Diamond’ jana alitoa msaada katika kituo cha watoto yatima cha Maunga Centre ambacho mwanamuziki TID anadaiwa kula fedha za yatima wanaoishi katika kituo hicho kilichopo Kinondoni Hananasif jijini Dar.

Akizungumza na mtandao huu kabla hajakabidhi msaada huo, Diamond alisema kuwa kikubwa zaidi kilichomfanya hadi atoe msaada huo ni kuguswa na maisha wanaoishi  yatima hao.
“Unajua siku zote Mungu anasema unachokipata ugawane na wenzako, sasa mimi pamoja na meneja wangu Joffrey a.k.a Joff tumeona tutoe nusu ya kile tulichokipata  kwa hawa ndugu zetu wanaolelewa katika kituo hiki,” alisema Diamond.…