flash3

Wednesday 9 May 2012

BEYONCE ASEMA ANAHITAJI WATOTO ZAIDI.

Mama wa mtoto mmoja Beyonce jumatatu alikuwa kwenye GLAMOROUS MET GALA huko New York, Kutoka Entertainment tonight Nancy O’Dell alimpiga Beyonce picha akiwa red carpet akiwa anafanya mahojiano, huku akiwa amevalia gauni refu jeusi. Beyonce mwenye miaka 30 alimuongelea mtoto wake wa miezi minne Blue Ivy Carter ambaye alikuwa nyumbani na baba yake Jay Z na mama yake Tina Knowles.Alisema anataka kuongeza mtoto mwingine kwenye familia lakini huenda isitokee siku za karibuni “Hata hivyo nataka watoto zaidi, sijui wangapi lakini Mungu ndo anajua” Alisema Beyonce. Beyonce atarudi kwenye satge kwa mara ya kwanza karibu mwaka sasa na series shows kwa dola bilioni 2.4 Revel Resort katika Memorial Day Weekend na show ya nne imewekwa kuwa Jumatatu Mei 28.

No comments:

Post a Comment