flash3

Friday 27 April 2012

Ni muda sasa mpango wa album kutoka kwa Fif haukuwa wazi kutokana na mambo kibao ambayo yanaendelea ndani ya label ya Interscope. Lakini katika mahojiano na waandishi wa habari mbali mbali katika club ya Floyd Mayweather pande za Las Vegas Fif alifunguka na kusema album itatoka july mwaka huu.
Akiwa katika ukumbi wa Floyd Mayweather Boxing club, pia Fif aliulizwa maswali kuhusu ndondi, alisema atachukua sehemu ya muda wake kufanya sports kama kijana, Pia aliongeza kwamba Mayweather ndo Mohammed Ally wa kizazi hiki ilifutiwa baada ya kuulizwa kama Mayweather ni mkali zaidi ya Mohammed Ally.
" Nimekuwa fan mkubwa wa ndondi , Nilianza ndondi nikiwa na umri wa miaka 12 lakini sikupata nafasi ya kufika mbali kama mshikaji wangu Mayweather ila napata faraja kupitia yeye, nadhani Mayweather ni kama Mohammed Ally wa kizazi hiki" Alifunguka 50 cent.

No comments:

Post a Comment