flash3

Friday 22 March 2013

PROFESA NA MWANDISHI WA VITABU "CHINUA ACHEBE" AFARIKI DUNIA AKIWA NA MIAKA 82

Nigeria yampoteza mtu muhimu sana 
Chinua Achebe, mwandishi wa vitabu, mwana mashairi anaejulikana sana Africa kutokana na kazi zake, hasa  kitabu kilichompa umaarufu sana "Things Fall Apart" amefariki dunia. Chinua amefariki  jana usiku akiwa na umri wa miaka 82, katika hospitali iliyoko Boston, Massachuttes, USA.

Premium Times imeripoti kuwa Professor Achebe amekuwa akiugua kwa mda mrefu ugonjwa ambao haukuzungumziwa.   Chebe alikua ni mwandishi wa vitabu vilivyompa umaarufu na vilivyoleta mapinduzi katika elimu ni pamoja na  Arrow of God, No Longer at Ease, Anthills of the Savannah, na A man of the People na kupokea tuzo mbali mbali za kitaifa kwa kazi zake.
Kitabu chake cha hivi karibuni ni "There was a county" ikiwa ni autobiography ya uzoefu wake na maoni yake juu ya vita vya wenyewe kwa wenyewe

Mpaka kifo kinamkuta, alikuwa ni profesa wa literature, Brown University.
REST IN ETERNAL PEACE 

No comments:

Post a Comment