flash3

Thursday 18 October 2012

MAINDA AFUNGUKA NA KUSEMA “UTOAJI WA MIMBA KWA WASANII WA BONGO MOVIE SASA NI KAMA FASHION”


Utoaji wa mimba kwa wasanii wa Bongo movie sasa ni kama fashion kwani usipofanya hivyo unaweza kuonekana mshamba wa mji, Mainda, ametoa ushahidi na kusema kuwa alishuhudia mwenyewe kwa macho yake mmoja wa mastaa wa kike wa Bongo movie akitoa mimba nyumbani kwake.

Msanii huyo akizungumza ,alidai kuwa wapo wasanii wengi wa tasnia hiyo ambao wanapata mimba lakini walio wengi wanazitoa. Alisema kuwa kwa upande wa msanii huyo hawezi kumtaja kwani baada ya kufanya kitendo kile alimuomba asitoe habari hiyo, hivyo ana heshimu maombi yake ingawa ni kitu cha hatari kwani mara baada kumaliza alipoteza fahamu na alikuja kurudi katika hali yake baada ya masaa kadhaa.

Hata hivyo kwa upande wake alihisi kama ameigia kwenye shimo lenye wadudu wakali kwani endapo kama kuna kitu chochote kingetokea siku hiyo yeye angekuwa ni muhusika wa kwanza kuwajibishwa kwani hakukuwa na mtu mwingine zaidi yake.

“Si kitu cha ajabu kwa wasanii wa Bongo movie kutoa mimba wapo wasanii wengi wanafanya hivyo, wapo watu wengi ambao wameshapoteza maisha kwa sababu ya kujaribu kutoa mimba na wengine kushindwa kuzaa kabisa, lakini bado watu wanaendelea na ujinga huo

No comments:

Post a Comment